• HABARI MPYA

    Saturday, February 22, 2014

    FLAMINI ALIVYOMTWANGA NGUMI WILSHERE BAADA YA KUZINGUANA MAZOEZINI JANA...NI SIKU CHACHE TU BADAA YA KUMPA MAKAVU OZIL

    KIUNGO Jack Wilshere ameposti picha inayomuonyesha akipigana na mchezaji mwenzake Mathieu Flamini baada ya mazoezi jana kwenye basi la timu.
    Viungo hao wawili walipigwa picha wakionekana kutofautiana kwenye mazoezi ya timu hiyo saa 24 kabla ya Arsenal kuwakaribisha Black Cats katika mchezo wa Ligi Kuu.
    Wote utani: Wilshere ameposti picha hii inayomuonyesha akipigana na Mfaransa huyo kwenye basi la timu
    Up for debate: Jack Wilshere and Mathieu Flamini exchange words
    Arm round the shoulder: Bacary Sagna with Wilshere in training
    Nipishe: Jack Wilshere amehusishwa na kutofautiana na mchezaji mwenzake Mathieu Flamini kwenye mazoezi ya Arsenal jana na Bacary Sagna anaonekana kwenda kusuluhisha
    Discussion: Wilshere stands with his arms open as Sagna looks to ease the apparent training ground tension
    Utaniambia nini: Wilshere akiongea kwa ishara ya mikono na Flamini huku Sagna akimfuata kumtuliza

    Bacary Sagna alijitolea kutuliza hasira za wawili hao kwa kumsihi Wilshere atulie.
    Lakini Wilshere akatweet kwa utani baadaye: "Flam hakufurahia wakati naondoka kwenye basi usiku! Samahani mwenzangu, naahidi kutotofautiana nawe tena!! #Hasira'
    Sakata la wachezaji hao wawili wa Arsenal linakuja siku kadhaa baada ya Flamini kutaka kugombana hadharani na Mesut Ozil wakifungwa mabao 2-0 na Bayern Munich Uwanja wa Emirates
    Kiungo huyo Mfaransa alimvaa Ozil akimtuhumu mchezaji huyo aliyenunuliwa kwa Pauni Milioni 42.5 kutojituma kwenye mechi hiyo.
    Arsenal wanarejea uwanjani leo kumenyana na Sunderland katika Ligi Kuu ya England wakitoka kutoa sare na Manchester United na kufungwa na Liverpool katika mechi zao mbili zilizopita.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: FLAMINI ALIVYOMTWANGA NGUMI WILSHERE BAADA YA KUZINGUANA MAZOEZINI JANA...NI SIKU CHACHE TU BADAA YA KUMPA MAKAVU OZIL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top