• HABARI MPYA

    Tuesday, December 03, 2013

    SIMBA YAANZA MAISHA MAPYA NA ZUNGU LAKE



    Na Dina Ismail, Dar es Salaam
    SIMBA SC imeanza maisha mapya chini ya kocha mpya, Mcroatia, Zdravko Lugarusic aliyeanza kuinoa timu jana akirithi mikoba ya Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibaden’, aliyefukuzwa baada ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Bara mwezi uliopita.
    Mwalimu huyo aliongoza mazoezi ya timu hiyo kwa mara ya kwanza jana Uwanja wa Kinesi, Dar es Salaam na miongoni mwa wachezaji waliohudhuria ni kipa mpya, Yaw Beko kutoka Ghana.
    Berko aliyewahi kuidakia Yanga SC alisani Mkataba wa miezi sita siku moja na Lugarusic, jana mbele ya Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe.
    Sera yangu ni ushindi na mataji; Kocha mpya Zdravco Lugarusic akizungumza na wachezaji jana Uwanja wa Kinesi.





    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA YAANZA MAISHA MAPYA NA ZUNGU LAKE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top