• HABARI MPYA

    Monday, December 30, 2013

    MOURINHO ASEMA SUAREZ ALICHEZA SARAKASI JANA, ALIJIRUSHA KWENYE BWALA LA KUOGELEA, RODGERS AMJIBU; "ETO'O ALIKUWA WA KULA NYEKUNDU NA KUSABABISHA PENALTI"

    KOCHA Jose Mourinho na Brendan Rodgers waliingia kwenye vita ya maneno jana baada ya mechi, ambayo Chelsea iliifunga Liverpool 2-1 katika Ligi Kuu y England.
    Samuel Eto’o alifunga bao la ushindi Uwanja wa Stamford Bridge, aikitumia makosa ya Simon Mignolet. 
    Lakini kocha wa Chelsea, Mourinho baadaye akamuita mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez mcheza sarakasi za kujirusha, kufuatia nyota huyo wa Uruguay kulalamika mara mbili kunyimwa penalti na refa Howard Webb baada ya kudhibitiwa kwenye eneo la hatari.
    Utata: Mshambuliaji wa Chelsea, Samuel Eto'o (kulia) akimdhibiti mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez katika eneo la penalti
    Contact: Eto'o's right leg appears to stop Suarez's determined chase of Cesar Azpilicueta
    Amemgusa: Mguu wa kulia wa Eto'o unaonekana ukimzuia Suarez asimfikie Cesar Azpilicueta anayekimbia na mpira 
    Ouch: Suarez screams in pain as he goes down in Chelsea's penalty area during the second half
    Suarez akiugulia maumivu huku akienda chini katika eneo la penalti la Chelsea kipindi cha jana
    Appeal: Suarez gestures for a penalty but is ignored by referee Howard Webb
    Penalti jamani: Suarez akililia penalti, lakini refa Howard Webb alimpuuza

    Mourinho alisema: "Hii ni nchi maalum. Mimi si Muingereza, lakini nahisi nina majukumu ya kutetea thamani fulani ya soka hii. 
    "Moja kati ya vitu vizuri tulivyonavyo ni hatupendi msisimko. Mazingira haya kwenye boksi, kwa Azpilicueta na Eto’o, yazuie au mpe kadi ya njano Suarez. Si nzuri kwa mchezo wetu. 
    Unimpressed: Chelsea manager Jose Mourinho believes Suarez deserved to be booked for his theatrics at Stamford Bridge
    Haijamvutia: Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho anaamini Suarez alistahili kuonyeshwa kadi ya njano kwa udanganyifu jana Uwanja wa Stamford Bridge
    Light-hearted? Mourinho and Liverpool's Suarez share a joke before the second-half begins
    Mourinho na Suarez walitaniana kidogo kabla ya kuanza kipindi cha pili jana
    Acrobatic: Mourinho accused Suarez of performing a 'swimming pool jump' after his side's 2-1 victory
    Sarakasi: Mourinho amemtuhumu Suarez kwa kucheza mchezo wa kujirusha kwenye bwawa la kuogelea baada ya timu yake kushinda 2-1

    "Eto’o aliingia ndani na ilionekana kama mtu fulani kampiga (Suarez) nyuma. Kwangu, ile ni kadi ya njano ya dhahiri. Alifanya mchezo wa kujirusha kwenye bwawa la kuogelea kujaribu kutafuta penalti, kwa sababu ni mweledi sana anajua yuko kwenye eneo la penalti na mashabiki wa Liverpool wapo nyuma yake. Ikiwa mchezaji wa Chelsea angefanya hivyo, ningemuambia usifanye hivyo,". 
    Quiet word: Referee Howard Webb speaks to Suarez but did not book the Uruguayan for simulation
    Amekosa maneno: Refa Howard Webb akizungumza na Suarez, lakini hakumpa kadi ya njano nyota huyo wa Uruguayan
    Going down: Suarez hits the ground after a tangle with Chelsea defender Gary Cahill
    Anaenda chini: Suarez akienda chini baada ya kukabiliana na beki wa Chelsea, Gary Cahill

    Rodgers, ambaye alikuwa rafiki wa karibu wa Mourinho, alijibu mapigo kwa kusema Eto’o alistahili kupewa kadi nyekundu kwa rafu aliyomchezea Jordan Henderson kwa sababu alimfuata na kumgonga mguuni, lakini hakupewa hata kadi ya njano 
    Na akasema pia kitendo cha Eto’o kumzinia njia Suarez kilistahili penalti.
    Mutual respect: Liverpool boss Brendan Rodgers (left) previously worked under Mourinho
    Heshima: Kocha wa Liverpool, Brendan Rodgers (kushoto) aliwahi kufanya kazi chini ya Mourinho awali
    Studs up: Rodgers believes Chelsea striker Eto'o should've seen red for this dangerous tackle on midfielder Jordan Henderon
    Rodgers anaamini mshambuliaji wa Chelsea, Eto'o alistahili kadi nyekundu kwa rafu mbaya aliyomchezea kiungo Jordan Henderon
    Impact: After getting away with his tackle on Henderson, Eto'o went on to score the winning goal for Chelsea
    Baada ya kunusurika katika rafu aliyomchezea Henderson, Eto'o akaenda kufunga bao la ushindi la Chelsea
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MOURINHO ASEMA SUAREZ ALICHEZA SARAKASI JANA, ALIJIRUSHA KWENYE BWALA LA KUOGELEA, RODGERS AMJIBU; "ETO'O ALIKUWA WA KULA NYEKUNDU NA KUSABABISHA PENALTI" Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top