• HABARI MPYA

    Thursday, December 19, 2013

    REAL MADRID WATAMBAA HADI 16 BORA KOMBE LA MFALME

    KLABU ya Real Madrid imefanikiwa kutinga hatua ya 16 Bora ya Kombe la Mfalme Hispania baada ya kuifunga Olimpic Xativa mabao 2-0 Uwanja wa Bernabeu.
    Kikosi cha Carlo Ancelotti walijiweka kwenye nafasi ngumu awali baada ya awali kutoa sare ya bila kufungana na timu hiyo ya Daraja la Kwanza.
    Lakini mabeki wa Real wakafanya kazi nzuri ya kutoruhusu mabao jana, huku Asier Illarramendi akiifungia timu hiyo bao la kwanza dakika ya 16 kabla ya Angel Di Maria kufunga la pili dakika ya 28 kwa penalti. Real sasa itakutana na Osasuna.
    Biashara imeisha: Carlos Casemiro na Angel di Maria wakipongezana kwa kuipa ushindi Real Madrid dhidi ya Olimpic de Xativa
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: REAL MADRID WATAMBAA HADI 16 BORA KOMBE LA MFALME Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top