• HABARI MPYA

    Sunday, December 29, 2013

    SIMBA WABORONGA USAJILI DIRISHA DOGO, TFF YABARIKI OKWI KUCHEZA YANGA, YAAHIDI KUFUATILIA FEDHA ZA KUUZWA TUNISIA

    Na Prince Akbar, Dar es Salaam
    KAMATI ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imekutana Jumamosi (Desemba 28, 2013) kujadili mambo mbalimbali yaliyofikishwa mbele yake ikiwemo usajili wa dirisha dogo ambapo klabu zenye matatizo zimepewa hadi Januari 10 mwakani kurekebisha.
    Donald Mosoti Omwanwa mmoja wa wachezaji wapya wa Simba SC
    Taarifa ya TFF, imesema baadhi ya klabu ikiwemo Simba zimezidisha idadi ya wachezaji, hivyo zimepewa hadi muda huo kupunguza ambapo zikishindwa kazi hiyo itafanywa na Kamati yenyewe.

    Simba ina nafasi tano za kujaza kwenye dirisha dogo lakini imewasilisha majina ya wachezaji sita.
    Pia klabu nyingine zimetakiwa ama kuvunja mikataba ya wachezaji au kuendelea kuwa nao, na si kuendelea kuwalipa mishahara wakati imeshawaondoa katika orodha yao.
    Kuhusu mshambuliaji Mganda, Emmanuel Okwi aliyesajiliwa Yanga, TFF imesema inafahamu kuwa klabu ya Simba bado haijalipwa fedha za kumuuza klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia na itasaidia kufuatilia FIFA fedha za mauzo ya mchezaji huyo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA WABORONGA USAJILI DIRISHA DOGO, TFF YABARIKI OKWI KUCHEZA YANGA, YAAHIDI KUFUATILIA FEDHA ZA KUUZWA TUNISIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top