• HABARI MPYA

    Thursday, December 19, 2013

    MAN UNITED WATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA LIGI, SPURS NJE LICHA YA ADEBAYOR KUFUNGA

    KOCHA David Moyes ameendelea kupambana baada ya jana kuiongoza Manchester United kushinda mabao 2-0 dhidi ya Stoke City katika Kombe la Ligi England.
    Ushindi huo wa United jana ulitokana na mabao ya Ashley Young dakika ya 61 na Patrice Evra dakika ya 78. 

    Raha ya bao: Ashley Young (kushoto) akishangilia baada ya kuifungia Manchester United bao la kwanza dhidi ya Stoke City

    Katika mchezo mwingine, mshambuliaji Emmanuel Adebayor alirejea uwanjani na kufunga bao moja wakati timu yake, Tottenham Hotspur ikifungwa 2-1 na West Ham United, mabao ya 
    Jarvis dakika ya 80 na Maiga dakika ya 85.
    Man United sasa itamenyana na Sunderland katika Nusu Fainali ya michuano hiyo maarufu kama Capital One, wakati West Ham itakipiga na Manchester City. 
    Adebayor akishangilia bao lake ambalo hata hivyo halikuweza kuinusuru Spurs na kipigo 

    Nayo Manchester City iliifunga 3-1 Leicester na kufikisha jumla ya mabao 75 katika mechi 25 za mashindano yote msimu huu. 
    Free-scoring: Sergio Aguero (centre) and Alvaro Negredo (left) are combining effectively in Manchester
    Free-scoring: Sergio Aguero (centre) and Alvaro Negredo (left) are combining effectively in Manchester
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED WATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA LIGI, SPURS NJE LICHA YA ADEBAYOR KUFUNGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top