• HABARI MPYA

    Thursday, March 22, 2012

    JUVE WALIMWA FAINI KWA UBAGUZI, MUNTARI KAWAPONZA


    Muntari
    KLABU ya Juventus imepigwa faini ya tatu msimu huu kwa vigezo, baada ya mashabiki wao kufanya hivyo Jumanne katika Nusu Fainali ya Kombe la Italia dhidi ya AC Milan.
    Mamlaka ya soka Italia imepiga faini ya euro 20 000, ambayo ni mara mbili ya waliyopigwa Juve January baada ya kumfanyia vitendo vya kibaguzi Mcolombia Pablo Armero wa Udinesena mzaliwai wa visiwa vya Cape Verde, anayechezea Usiwsi, Gelson Fernandes.
    Pia walipigwa faini ya euro 10 000, Oktoba baada ya kufanyiwa vitendo hivyo dhidi ya Inter Milan.
    Kiungo wa Milan, Sulley Muntari wa Ghana na Mholanzi Urby Emanuelson ndio waliofanyiwa vitendo hivyo vya ubaguzi Jumanne.
    Ubaguzi huu unawafanya mashabiki wa Juventus wawe wamekubuhu kwa tabia hiyo. Walimfayia hivyo mshambuliaji wa Manchester City, Mario Balotell alipokuwa Inter.
    Msimu wa 2008/2009 Juve walilazimika kucheza mechi katika Uwanja usio na mashabiki baada ya mashabiki wao kumfanyia ubaguzi Balotelli katika mechi dhidi ya Inter.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JUVE WALIMWA FAINI KWA UBAGUZI, MUNTARI KAWAPONZA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top