TIMU ya Zamalek SC ya Misri imefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika baada ya ushindi wa mabao 2-1 na AS Otoho d'Oyo ya Kongo-Brazzaville katika mchezo wa marudiano wa Robo Fainali jana Uwanja wa Cairo International Jijini Cairo nchini Misri.
Kwa matoke ohayo, Zamalek inakwenda Nusu Fainali kwa ushindi wa jumla wa 3-2 kufuatia sare ya kufungana bao 1-1 katika mchezo wa kwanza Machi 14 Uwanja wa Alphonse Massamba-Débat Jijini Brazzaville.
Mambo hayakuwa mazuri kwa timu za Wydad Athletic ya Morocco na AS Maniema Union ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ambazo zote zilitolewa kwa mabao ya ugenini zote.
Wydad Athletic ilitoa sare ya kufungana mabao 2-2 na Olympic Club de Safi, zote za Morocco jana Uwanja wa Mfalme Mohammed wa Tano Jijini Casablanca.
Kwa matokeo hayo, Olympic Club de Safi inakwenda Nusu Fainali kwa faida ya mabao ya ugenini katika sare hiyo ya jumla ya 3-3 baada ya awali timu hizo kufungana bao 1-1 kwenye mchezo wa kwanza Machi 16 Uwanja wa El Massira mjini Safi.
Nayo AS Maniema Union ilichapwa 1-0 USM Alger bao pekee la kiungo Brahim Benzaza dakika ya 30 Uwanja wa Julai 5, 1962 Jijini Algiers nchini Algeria.
USM Alger inakwenda Nusu Fainali kwa faida ya mabao ya ugenini katika sare hiyo ya jumla ya 2-2 kufuatia kufungwa 2-1 na AS Maniema Union kwenye mchezo wa kwanza wa Robo Fainali Machi 15 Uwanja wa TP Mazembe Jijini Lubumbashi.
Mechi za kwanza za Nusu Fainali zitachezwa Aprili 10 na marudano Aprili 17, Zamalek ikimenyana na CR Belouizdad iliyoitoa Al Masry ya Misri pia na USM Alger ikicheza na Olympic Safi.



.png)
0 comments:
Post a Comment