• HABARI MPYA

    Tuesday, December 03, 2013

    SUDAN KUSINI YA KWANZA KUAGA CHALLENGE, MUNGU IBARIKI ZANZIBAR IIBUTUE KENYA JIONI HII AFRAH

    Na Mahmoud Zubeiry, Nairobi
    SUDAN Kusini imekuwa timu ya kwanza kuyaaga rasmi mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge baada ya kufungwa mabao 2-0 na Ethiopia katika mchezo wa Kundi A, uliofanyika Uwanja wa Afrah mjini Nakuru, Kenya.
    Shukrani kwao Yousuf Yassin aliyetokea benchi kipindi cha pili na kufunga bao la kwanza dakika ya 54 baada ya kupokea pasi nzuri ya Manaye Fantu kutoka upande wa kulia na Biruk Kalbolre aliyeingia pia ngwe ya pili aliyefunga dakika ya 82.
    Beki wa Sudan Kusini, Clement Badru kushoto akiwa amempiga kwanja mshambuliaji wa Ethiopia, BereketYisak leo Uwanja wa Afrah
    Kwa matokeo hayo, taifa hilo jipya liliojitenga kutoka Sudan, linaaga mashindano hayo bila kuwa na pointi hata moja, baada ya kufungwa pia mechi zake mbili za awali, 2-1 dhidi ya Zanzibar na 3-1 na Kenya.
    Ethiopia inamaliza kileleni mwa Kundi A kwa pointi zake saba, baada ya kuwafunga pia na Zanzibar 3-1 na kutoka sare tasa na Kenya.

    Mechi ifuatayo baina ya wenyeji Kenya, Harambee Stars na Zanzibar itatoa mustakabali zaidi wa kundi hilo juu  timu zitakazosonga Robo Fainali.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SUDAN KUSINI YA KWANZA KUAGA CHALLENGE, MUNGU IBARIKI ZANZIBAR IIBUTUE KENYA JIONI HII AFRAH Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top