• HABARI MPYA

    Saturday, December 22, 2012

    YANGA WAMPA MTU 4-0, KINDA LA B LAPIGA HATTRICK

    Kocha wa Yanga, Ernie Brandts

    Na Prince Akbar
    YANGA SC jana imeitandika mabao 4-0 Kijitonyama Stars katika mchezo wa kirafiki kwenye Uwanja wa Kijitonyama, Dar es Salaam.
    Mabao ya Yanga jana yalifungwa na George Banda matatu na Rehani Kibingu moja, ambao wote wamepandishwa kutoka timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20.

    Kikosi cha Yanga jana kilikuwa mseto; Ally Mustafa ‘Barthez’/Said Mohamed, Juma Abdul/Nssajigwa Shadrack, Oscar Joshua/Stefano Mwasyika, Ladislaus Mbogo/Job Ibrahim, Mbuyu Twite, Nurdin Bakari, Rehani Kibingu/Godfrey Taita, Kabange Twite, Jerry Tegete/Omega Seme, George Banda na David Luhende.
    Yanga inaendelea na mazozi mjini Dar es Salaam kujiandaa na safari yake ya Uturuki wiki ijayo ambako inakwenda kuweka kambi ya wiki mbili. Kikosi cha Yanga kinatarajiwa kuwa kamili kesho, baada ya wachezaji wake wengine kumaliza majukumu yao ya kitaifa leo, katika mechi kati ya Tanzania na Zambia leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: YANGA WAMPA MTU 4-0, KINDA LA B LAPIGA HATTRICK Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top