• HABARI MPYA

    Friday, December 21, 2012

    KIIZA AWASILI YANGA

    Kiiza

    Na Prince Akbar
    MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uganda, Hamisi Kiiza ‘Diego’ amewasili jana Dar es Salaam jana kujiunga na timu yake, Yanga SC baada ya mapumziko kufuatia mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge.
    Kiiza aliyeiongoza Uganda kutwaa ubingwa mjini Kampala, Uganda aliomba mapumziko baada ya Kombe la Challenge na jana amerejea rasmi kazini.
    Yanga inatarajiwa kwenda kuweka kambi Uturuki, Desemba 28, mwaka huu kujiandaa na Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame pamoja na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
    Kikosi kizima cha Yanga kipo kambini Dar es Salaam, kikijifua vikali chini ya kocha wake Mkuu, Mholanzi Ernie Brandts.
    Yanga imepania kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu pamoja na kutetea Kombe la Kagame, michuano ambayo itafanyika Januari mwakani mjini Kigali, Rwanda.       
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: KIIZA AWASILI YANGA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top