• HABARI MPYA

    Saturday, March 24, 2012

    KOCHA SETIF ASEMA AKILI YAO KOMBE LA SHIRIKISHO SI SIMBA

    Setif wakiwa Uwanja wa Karume baada ya mazoezi juzi
    KOCHA mkuu wa ESS Setif ya Algeria, Geiger Alain, amesema wameamua kufanya mazoezi kwenye jua kali ili kuendana na hali ya hewa ya Tanzania.
    Alain alisema pia kuwa, mazoezi wanayofanya siyo kwa ajili ya kupambana na Simba tu, bali ni kusonga mbele kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho.
    Kauli hiyo imekuja kufuatia kufanya mazoezi kwenye jua kali asubuhi na jioni.
    Alisema kwa kawaida wao hufanya mazoezi kila siku asubuhi hata kama wana mechi siku hiyo, lakini kutokana na kutoizoea hali ya hewa ya Dar es Salaam, wameamua kufanya muda huo ili waweze kumudu kucheza.
    "Tunafanya mazoezi wakati wa jua kali ili tuweze kuzowea baada ya kuona joto linatuchosha sana hivyo tusipojipanga tunaweza kukosa pumzi siku ya mechi yetu," alisema.
    Simba na ES Setif zitashuka dimbani kesho katika mechi ya kwanza raundi ya pili kuwania Kombe la Shirikisho kwenye Uwanja wa Taifa.
    Simba imepata nafasi hiyo baada ya kuindoa kwenye michuano Kiyovu ya Rwanda.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KOCHA SETIF ASEMA AKILI YAO KOMBE LA SHIRIKISHO SI SIMBA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top