• HABARI MPYA

    Saturday, March 24, 2012

    MILOVAN ATOA WOSIA WA MWISHO SIMBA

    
    Milovan, kocha wa Simba
    WAKATI homa ya pambano la kimataifa kati ya Simba na Es Setif ya Algeria ikizidi kupamba moto, kocha mkuu wa wekundu hao Mserbia Curkovic Milovan amewataka mabeki wake Juma Nyoso na Kelvin Yondan na Amir Maftah kuwa makini zaidi kwani wana kazi kubwa ya kuzuia mipira ya juu na kona ambayo imekua ikitumiwa sana na wapinzani wao. Milovan ambaye katika mazoezi ya juzi alionekana zaidi akiwapa mbinu mabeki hao kwa kuwafundisha jinsi ya kupambana na mipira ya juu pamoja na kona, amewataka kuongeza umakini katika eneo lao. Katika mazoezi hayo, Milovan aliwatumia Uhuru Seleman na Salum Machaku kupiga mipira ya kona ili kuwapa uzoefu mabeki jinsi ya kucheza na kuokoa mipira hiyo. "Tumejiandaa vizuri na wachezaji wote wako katika hali nzuri, kiufundi timu ipo katika kiwango cha kuridhisha ingawa nilikua nikiwapa mbinu zaidi mabeki ambao naamini wana kazi kubwa," alisema Milovan. Aidha kwa upande wa washambuliaji Okwi, Mafisango na Felix Sunzu nao walikua wakipewa kazi ya ziada ya kuhakikisha wanamiliki mipira na kufunga mabao ya haraka.  Akizungumza hali ya Juma Jabu ambaye ni majeruhi, alisema huenda nafasi yake ikachezwa na Amir Maftah ambaye naye jana alikuwa akipatiwa mazoezi ya aina yake. Wakati Milovan akiwapa wachezaji wake mbinu hizo, kocha wa Setif, Geiger Alain kwenye mazoezi ya timu yake Uwanja wa Karume alikuwa akiweka mkazo washambuliaji wake kufunga mabao mengi. Milovan atalazimika kutafuta mbinu bora haraka ili kuzuia mashambulizi ya hatari ya kipindi cha pili kutoka kwa ES Setif kwa ajili ya kujihakikisha matokeo mazuri. Udhaifu mkubwa Simba msimu huu upo katika kipindi cha pili, ambapo wanaonekana kuchoka na kuruhusu mashambulizi mengi langoni mwao jambo lililofanya mpaka sasa kufungwa mabao 9 kati ya 14 katika muda huo. Rekodi hiyo mbaya ya kiuchezaji iliyoonyeshwa na Simba msimu huu itakuwa ni faida kubwa kwa wapinzani wao ES Setif waliojijengea utamadumi wa kupata ushindi katika kipindi cha pili. Simba walifika fainali katika mashindano ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika mwaka 1993, ambapo ilicheza mechi ya kwanza na Stella Club na kutoka suluhu 0-0 nchini Ivory Coast na zilirudiana nchini Tanzani, timu ya Simba ilifungwa 2-0 na Stella kutwaa ubingwa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MILOVAN ATOA WOSIA WA MWISHO SIMBA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top