• HABARI MPYA

    Wednesday, October 31, 2012

    YANGA B WAITILIA UBANI YANGA A, WAYACHAPA KIDUDE MAKINDA YA MGAMBO


    Timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Yanga, imeifunga Mgambo JKT ya vijana pia, bao 1-0 katika mchezo wa utangulizi, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, kabla ya kuanza kwa mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baina ya kaka zao, Yanga A dhidi ya Mgambo JKT ya Handeni, Tanga. Bao hilo pekee lilitiwa kimiani na Clever Charles dakika ya 65.
    Zuberi Amiri wa Yanga B, akichuana na Charles Domayo wa JKT Mgambo

    Joseph Banda wa Yanga B (25) akipasua ukuta wa Mgambo

    Meshack Ramadhani wa Yanga kushoto akigombea mpira na beki wa Mgambo

    Banda akifumua shuti mbele ya mabeki wa Mgambo, mmoja akijaribu kuzuia

    Notikel Masasi wa Yanga B akiwa chini ya ulinzi wa mabeki wa Mgambo

    Kocha Ernie Brandts akifuatilia vipaji Yanga B ikicheza na Mgambo

    Notikel Masasi wa Yanga B, akichuana na mchezaji wa Mgambo

    Clever Charles, mfungaji wa bao la Yanga B leo, akiwa benchi baada ya kupumzishwa. Kulia kwake ni Said Manduta.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: YANGA B WAITILIA UBANI YANGA A, WAYACHAPA KIDUDE MAKINDA YA MGAMBO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top