• HABARI MPYA

    Monday, October 29, 2012

    UCHAGUZI DRFA JIRANI KABISA NA UCHAGUZI WA TFF

    Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Soka Dar es Salaam (DRFA), Juma Simba ‘Gadaffi’ (katikati) akizungumza na Waandishi wa Habari leo, kwenye ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) juu ya uchaguzi wa chama hicho. Simba amesema uchaguzi wa DRFA utafanyika Desemba 8, mwaka huu na fomu za kugombea nafasi mbalimbali zitaanza kutolewa kesho. Novemba 4 hadi 8, Kamati yake itapitia fomu za walioomba uongozi, Novemba 9 hadi 13 utakuwa muda wa pingamizi kwa wagombea, ambazo zitajadiliwa Novemba 14 hadi 16, wakati Novemba 17 hadi 19 watatoa fursa ya kukata rufaa, ambazo zitasikilziwa Novemba 20 hadi 24 na baada ya hapo, Novemba 25 yatatangazwa majina ya wagombea waliopitishwa. Tarehe hii mpya ya uchaguzi wa DRFA inaufanya usogeleane na uchaguzi wa TFF, ambao utafanyika pia Desemba.   

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: UCHAGUZI DRFA JIRANI KABISA NA UCHAGUZI WA TFF Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top