• HABARI MPYA

    Monday, October 22, 2012

    ONYESHO LA TWANGA PEPETA LILIVYOFANA MZALENDO PUB JANA

    Onyesho maalum la bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ kwa mashabiki wake wa Facebook, lililopewa jina Twanga Pepeta Facebook Party lilifana jana kwenye ukumbi wa Mzalendo Pub, Kijitonyama, Dar es Salaam kwa burudani nzuri iliyoporomoshwa na bendi hiyo. Pamoja na burudani nzuri, blogs za Issa Michuzi, Jiachie, Full Shangwe, Millard Ayo, BIN ZUBEIRY na Global Publisher zilipewa tuzo za kutambuliwa kwa mchango wao, kwenye mafanikio ya bendi hiyo, ambavyo vilitolewa na Mwenyekiti wa Africans Stars Entertainment (ASET), Baraka Msilwa, wamiliki wa bendi hiyo. Tazama mapicha ya BIN ZUBEIRY ukianza na hiyo ya kufunguliwa shampeni na jamaa anayeitwa Hemedi 'Young Milionea'.

    Kulia Prince Muumin Mwinjuma akiimba na Luiza Mbutu kushoto


    Dogo Rama kulia akifanya vitu vyake na mwanamuziki mwenzake
    Mashabiki wa Twanga

    Mashabiki wakicheza sebene la Twanga

    Sijui walikuwa wanafanya nini wanenguaji hawa wa Twanga kwenye eneo la kuegeshea magari

    Msemaji wa Twanga Pepeta, Muddy Pizzaro akimiminiwa shampeni na Queen Suzy wa FM Academia ambaye alikuwa mmoja wa waalikwa

    Mastaa wa Bongo Movie JB, Ray na Hartman walikuwepo

    Wanamuziki wa Twanga Pepeta wakiwa na rafiki yao

    Nyoshi El Saadat akiimba kwenye jukwaa la Twanga jana kama mmoja wa waalikwa 

    Swaga za Sharapova, mnenguaji wa Twanga Pepeta

    Queen Suzzy katikati anafungua shampeni, kuliwa Baraka Msilwa na kushoto Muddy Pizzaro

    Jembe likifuatilia kwa makini shoo

    Kulia Kalala Junior, anayemfuatia Steve Nyerere na wa mwisho ni Deo Mutta 'Mwana Twanga'

    Wanenguaji wa kiume wa Twanga Pepeta

    Baraka Msilwa baada ya kunikabidhi tuzo ya kuheshimu mchango wangu katika mafanikio ya bendi yao

    Nikisoma cheti kwa chati pembeni ya Baraka Msilwa, kaka wa siku nyingi Dar es Salaam

    Wanenguaji wa Twanga Pepeta

    Mnenguaji wa Twanga Pepeta akifanya mambo

    Menguaji wa Twanga Pepeta akionyesha umahiri wake

    Mnenguaji wa Twanga 'akiua' 

    Wanenguaji wa Twanga Pepeta, wakicheza rap moja ya zamani ya bendi hiyo, I Love You Baby

    Wakicheza I Love You Baby...

    Wanenguaji wa Twanga Pepeta 

    Waimbaji kutoka kushoto Muumini, Janet Isinike...

    Waimbaji

    Janet Isinike 'janet Jackson' na Dogo Rama

    Luiza Mbutu na Saleh Kupaza
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ONYESHO LA TWANGA PEPETA LILIVYOFANA MZALENDO PUB JANA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top