Kell Brook ametimiza ndoto zake za kuwania ubingwa wa dunia, baada ya jana usiku kumtwanga Muargentina Hector Saldivia katika raundi ya tatu kwenye ukumbi wa Motorpoint Arena mjin Sheffield.
Bondia huyo Muingereza mwenye umri wa miaka 26, alionekana kumzidi mpinzani wake kuanzia kengele ya kwanza katika pambano lake la mwisho la mchujo kabla ya kuwania taji la IBF, uzito wa Welter ambalo anapenda kuligombea mapema mwakani.
Brook aliahidi kumtandika Saldivia ili kuilipia timu ya taifa ya soka ya England kisasi cha bao la Mkono wa Mungu la Maradona.

Kell Brook kulia akizipiga na Hector Saldivia

Brook akimpa kitu Saldivia

Brook amemkalisha chini Saldivia

Brook amemmaliza Saldivia kwa kumkalisha chini

Brook akishuhudia mpinzania wake akihesabiwa na refa Howard Foster

Brook akishangilia na mwalimu wake

Sasa ni mshindani Namba 1: Brook akishangilia na promota wake Eddie Hearn


.png)