• HABARI MPYA

    Friday, March 23, 2012

    WAPENDA FUJO SIYO KWETU TU, HATA KENYA WAPOOOOOOOO


    BODI ya Viwanja vya Michezo (SSMB) imeifungia klabu ya Gor Mahia kutumia viwanja vya Nyayo na Moi International Sports Centre Kasarani.
    Hatua hiyo inakuja baada ya vurugu za mwishoni mwa wiki katika mechi yao na wapinzani wao wa jadi, AFC Leopards ambayo ilivunjika baada ya dakika 26 tu.
    Uamuzi huo umefikiwa leo na kutangazwa na Mwenyekiti wa bodi, Generali Mstaafu Daniel Opande.
    Pamoja na hayo, uamuzi hao haupokewa vizuri na Gor Mahia ambayo imechukuliwa kama ni wa haraka.
    Kifungo hicho kinawafanya Gor wawe na Uwanja mmoja tu wa kutumia, City ambao hauendani na idadi kubwa ya mashabiki wao
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WAPENDA FUJO SIYO KWETU TU, HATA KENYA WAPOOOOOOOO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top