![]() |
| Pepe kushoto akifanya viktu vyake vinavyomponza mara kwa mara. Hapa anamtandika teke Puyol wa Barcelona. |
BEKI mchapa kiatu wa Real Madrid, Pepe amefungiwa mechi
mbili za Ligi Kuu ya Hispania, La Liga kwa kumtukana refa katika mechi waliyolazimishwa
sare ya 1-1 Ijumaa na Villarreal.
Mwenzake Sergio Ramos, hata hivyo aliponyoka adhabu kubwa
baada ya adhabu ya kadi ya njano aliyoonyeshwa siku ya jumatano kupuuzwa na
Kamati ya shirika la mpira la Uhispania.Beki huyu Mreno wa Real Madrid anaweza kucheza mechi ya leo na Real Sociedad.
Kocha Jose Mourinho na kiungo Mjerumani, Mesut Ozil walionyeshwa kadi nyekundu wakati wa pambano hilo, baada ya Villarreal kupata bao la kusawazisha dakika za lala salam, nao wamefungiwa mechi moja kila mmoja.
Kocha Msaidizi wa Mourinho, Rui Faria amefungiwa mechi mbili baada ya kutolewa nje katika kipindi cha pili Uwanja wa El Madrigal.



.png)
0 comments:
Post a Comment