• HABARI MPYA

    Wednesday, June 03, 2015

    XAVI ASHINDWA KUZUIA MACHOZI KATIKA 'PATI' LA KUMUAGA CAMP NOU

    MKONGWE, Xavi ameshindwa kuzuia hisia zake na kumwaga machozi wakati shamrashamra za kumuaga Barcelona kuelekea fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Juventus.
    Xavi amemshukuru kocha Luis Enrique kwa kumuwezesha kubaki katika klabu hiyo msimu uliopita.
    Kiungo huyo anayeondoka, alitangaza mwezi uliopita kwamba anakwenda kumalizia soka yake katika klabu ya Al-Sadd ya Qatar mwishoni mwa msimu, akihitimisha miaka yake 24 kuwa na vigogo hao wa Katalunya.
    Kuelekea fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Juventus, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 35 alipewa heshima katika klabu ambayo aliitumikia kwa muda mrefu tangu ana umri wa miaka 11 alipojiunga nayo.
    Barcelona star Xavi (left) was joined by team-mate Andres Iniesta in his farewell event at the Nou Camp
    Nyota wa Barcelona, Xavi (kushoto) akifuta machozi pembeni ya mchezaji mwenzake, Andres Iniesta wakati shamra shamra za kuagwa Uwanja wa Nou Camp leo PICHA ZAIDI GONGA HAPA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: XAVI ASHINDWA KUZUIA MACHOZI KATIKA 'PATI' LA KUMUAGA CAMP NOU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top