• HABARI MPYA

    Tuesday, June 23, 2015

    MESSI AULA COPA AMERICA, SANCHEZ WA ARSENAL SI LOLOTE!

    The two Argentinian forwards share a joke during training ahead of their quarter-final against Colombia
    Mwanasoka wa kimataifa wa Argentina, Lionel Messi yumo kwenye kikosi bora cha hatua ya makundi Copa America

    KIKOSI BORA CHA HATUA YA MAKUNDI COPA AMERICA 

    Bravo (Chile); Silva (Brazil), Gimenez (Uruguay), Medel(Chile); Aranguiz (Chile), Lobaton (Peru), Sanchez(Colombia), Vidal (Chile); Aguero (Argentina), Barrios(Paraguay), Messi (Argentina) 
    NYOTA wa Barcelona, Lionel Messi na Manchester City, Sergio Aguero wanaongoza orodha ya kikosi cha wachezaji 11 bora wa hatua y amakundi michuano ya Copa America.
    Nyota hao, wapo pamoja na kiungo mtata wa Chile, Arturo Vidal ambaye wiki iliyopita akiwa 'mitungi' aliligongesha gari lake aina ya Ferrari nyekundu lenye thamani ya Pauni 230,000, kabla ya kuripotiwa 'kuwabwatukia' Maofisa wa Polisi ambao walimuweka rumande. 
    Lakini anawania ufungaji bora wa mashindano baada ya hatua ya makundi, wakati mshambuliaji wa Arsenal, Alexis Sanchez, licha ya Chile wenyeji wa Copa America ya mwaka huu kufanya vizuri, hayumo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MESSI AULA COPA AMERICA, SANCHEZ WA ARSENAL SI LOLOTE! Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top