• HABARI MPYA

    Sunday, May 26, 2013

    ROONEY AITWA FARAGHA NA MOYES ATULIZWE ABAKI MAN UNITED


    IMEWEKWA MEI 26, 2013 SAA 1:40 ASUBUHI
    MSHAMBULIAJI Wayne Rooney anatarajiwa kuwa kikao maalum na kocha mpya wa Manchester United, David Moyes kama sehemu ya juhudi za klabu kutatua tatizo la nyota huyo wa England juu ya mustakabali wake baada ya kutofautiana na kocha aliyeondoka, Sir Alex Ferguson. 
    Wakati Moyes anajiandaa kwa sikukuu ya kifamilia na Rooney yupo kwenye majukumu ya timu ya taifa ya England  wiki hii, inafahamika kwamba wote wapo tayari kukutana haraka iwezekanvyo kutatua mustakabali wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27, Rooney. 
    Klabu sasa imekubali Rooney hajawahi kutoa maombi ya kuondoka na pamoja na hayo, Moyes atataka kukutana na mchezaji huyo binafsi kabla ya uamuzi wa mwisho kufikiwa. Rooney anataka kubaki katika klabu hiyo na Moyes anamkubali mchezaji huyo. 
    Ringside: Manchester United striker Wayne Rooney was at the O2 Arena on Saturday night
    Pembeni ya ulingo: Mshambuliaji wa Manchester United, Wayne Rooney alikuwa kwenye Uwanja wa O2 Arena jana usiku kuangalia ndondi
    Wayne Rooney
    David Moyes
    Makofi: Wayne Rooney atakutana na David Moyes kujadili mustakabali wake Manchester United
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ROONEY AITWA FARAGHA NA MOYES ATULIZWE ABAKI MAN UNITED Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top