• HABARI MPYA

    Wednesday, May 29, 2013

    MOYES ATAKA KUMSAJILI FABREGAS MAN UNITED...BARCA WAKO TAYARI KUMUUZA, MCHAWI ARSENAL TU

    IMEWEKWA MEI 29, 2013 SAA 10:00 JIONI
    KOCHA mpya wa Manchester United, David Moyes anataka mchezaji wake wa kwanza kumsajili, awe kiungo wa zamani wa Arsenal, Cesc Fabregas.
    Kocha huyo mpya wa Mashetani Wekundu anataka mchezeshaji huyo atue Old Trafford kumaliza tatizo la safu ya kiungo la Manchester United na klabu yake ya sasa, Barcelona iko tayari kumuuza nyota huyo wa Hispania.
    Huku Paul Scholes akistaafu na Anderson kushindwa kumaliza tatizo la safu hiyo, Fabregas anaweza kuwa suluhisho kwa mabingwa hao.
    Aiming high: David Moyes wants to bring Cesc Fabregas back to the Premier League
    David Moyes anataka kumsajili Cesc Fabregas arejee Ligi Kuu England

    Arsenal walipewa kipaumbele cha kumsajili tena Fabregas wakati atakapoondoka Barcelona, lakini Manchester United wanajiamini wataizidi nguvu Gunners kwa ushawishi wa kifedha.
    If you can't beat them... Fabregas would replace Paul Scholes in the heart of the team
    Fabregas anaweza kuchukua nafasi ya Paul Scholes katika moyo wa timu
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MOYES ATAKA KUMSAJILI FABREGAS MAN UNITED...BARCA WAKO TAYARI KUMUUZA, MCHAWI ARSENAL TU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top