Mjumbe wa Kamati ya Mashindano ya Simba SC, Abdulfatah Salim Saleh
akimkabidhi zawadi ya jezi ya Simba SC, mshambulaji wa Al Nasir ya Sudan, Kun
James baada ya kukoshwa na soka yake Jumamosi, timu hiyo ilipocheza na Azam FC na
kulala 3-1 katika Kombe la Shirikisho Afrika. James ambaye pia anachezea timu
ya taifa ya Sudan Kusini, ndiye aliyekuwa akiisumbua mno ngome ya Azam siku
hiyo na ndiye aliyetoa pasi ya bao la Nasir, lililofungwa na Fabian Elias.
James ametua Nasir msimu huu akitokea El Merreikh ya Sudan,
aliyoichezea kuanzia mwaka 2010, alipojiunga nayo akitokea El Gouz iliyomuibua
mwaka 2007.
James mwenye umri wa miaka 25, anasema anapenda kucheza nje
ya kwao na yuko tayari kusaini timu yoyote ya hapa Tanzania itakayomuhitaji.
|