• HABARI MPYA

    Thursday, June 04, 2015

    BARCELONA WAWASHA MOTO BAADA YA FIGO KUITIWA JEZI YAO, WAIAMBIA UEFA ISITHUBUTU!

    KLABU ya Barcelona imekataa kuwakilishwa na Luis Figo katika mchezo wa magwiji mjini Berlin, Ujerumani Ijumaa.
    Figo aliyecheza kwa miaka mitano Nou Camp kabla ya kuhamia Real Madrid mwaka 2000, ameteuliwa na UEFA katika kombaini ya wachezaji wa zamani wa Juventus na Barcelona watakaomenyana na timu ya Dunia. 
    Pamoja na hayo, Barcelona imeitaka UEFA kumuondoa Figo kwenye timu yao ili kutowakera mashabiki, ambao kwa miaka 15 sasa bado wana hasira baada ya mchezaji huyo kuihama klabu hiyo kwa utata.
    Figo (in action against Chelsea) was a key part of the Barcelona team before he left for Real Madrid
    Luis Figo (akiichezea Barca dhidi ya Chelsea) alikuwa tegemeo la Barcelona kabla ya kuhamia Real Madrid

    Figo, ambaye sasa anafikiria kugombea tena Urais wa FIFA, aliisaidia Barcelona kutwaa mataji mawili ya La Liga kabla ya kuhamia Real Madrid kwa dau la rekodi wakati huo, Pauni Milioni 37.
    Uhamisho huo uliwakera mashabiki wa Barcelona na wakati Figo aliporejea na Real kucheza Uwanja wa Nou Camp kwa mara ya kwanza Oktoba mwaka 2000 wa,limzomea Mreno huyo. 
    Figo akajibu kwa kuziba vidole masikioni mwake, kuwapa ishara kwanza hasikii kelele zao, jambo ambalo liliongeza hasira za mashabiki hao. 
    Figo moved to Real Madrid for a then world record fee of £37.5m in a move that shocked football
    Figo alihamia Real Madrid kwa dau la rekodi wakati huo Pauni Milioni 37.5, uhamisho ambao uliishitua dunia
    Figo cups his hears as he sends a message to the booing Barcelona fans on his first return to the Nou Camp 
    Figo akiwa ameziba masikio yake kuwabeza mashabiki wa Barcelona waliokuwa wanamzomea Uwanja wa Nou Camp 
    A pig's head was thrown on to the pitch during the 2002 derby - Figo's second return to the Nou Camp 
    Kichwa cha nguruwe kilirushwa Uwanja wa Nou Camp mwaka 2002 wakati Figo aliporejea kwa mara ya pili na Real kucheza na mahasimu, Barcelona

    Mara ya pili aliporejea Nou Camp mwaka mmoja baadaye, kichwa cha nguguruwe kilirushwa uwanjani na kusababisha mchezo kusimama kwa dakika 20 wakati mashabiki wakitupa makopo ya bia, mioto na chupa kutoka jukwaani.   
    Pamoja na hayo, Figo akawakata maini Bernabeu kwa kuisaidia Real kutwaa ubingwa mwaka 2001 na akashinda tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka wa Dunia. Mwaka uliofuata akashinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulayana lingine la La LIga kabla ya kuhamia Inter Milan kama mchezaji huru mwaka 2005. 
    Mechi ya magwiji Ijumaa itawachanganya wachezaji wa zamani wa Juventus na Barcelona katika kikosi kimoja kuelekea Fainali ya Ligi ya Mabingwa baina ya mabingwa hao wa Italia na Hispania. Kikosi cha Juventus na Barcelona kitakuwa chini ya makocha Ruud Gullit na Peter Schmeichel wakati Zico atakuwapo pia. 

    VIKOSI VYA MCHEZO HUO..

    MAGWIJI WA JUVENTUS NA BARCELONA: Edwin van der Sar, Ciro Ferrara, Ludovic Giuly, Alessandro Del Piero, Giovanni van Bronckhorst, Edmílson, Fabio Cannavaro, David Trezeguet, Mark van Bommel, Gianluca Zambrotta, Deco, Eric Abidal, Christian Vieri
    NYOTA WA DUNIA: Jens Lehmann, Cafu, Youri Djorkaeff, Robert Pires, Predrag Mijatović, Giovane Elber, Clarence Seedorf, Rai, Christian Karembeu, Steve McManaman, Pierre van Hooijdonk, Marco Materazzi
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BARCELONA WAWASHA MOTO BAADA YA FIGO KUITIWA JEZI YAO, WAIAMBIA UEFA ISITHUBUTU! Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top