Na Mahmoud Zubeiry, RUSTENBURG
MICHUANO ya Kombe la Mataifa ya kusini mwa Afrika COSAFA, mwaka 2015 inaanza kesho mjini hapa, Rustenburg, jimbo la Kaskazini Magharibi, Afrika Kusini.
Michuano hiyo ya 15 itashirikisha timu 14, zikiwemo mbili, Tanzania na Ghana wageni waalikwa. Timu nyingine ni Mauritius, Shelisheli,
Swaziland, Madagascar, Zimbabwe, Namibia,
Lesotho , Botswana, Malawi, Msumbiji, Zambia na wenyeji Afrika Kusini.
Kundi A lina timu za Namibia, Mauritius, Shelisheli na Zimbabwe, wakati Kundi B lina timu za Lesotho, Madagascar, Swaziland na Tanzania.
MICHUANO ya Kombe la Mataifa ya kusini mwa Afrika COSAFA, mwaka 2015 inaanza kesho mjini hapa, Rustenburg, jimbo la Kaskazini Magharibi, Afrika Kusini.
Michuano hiyo ya 15 itashirikisha timu 14, zikiwemo mbili, Tanzania na Ghana wageni waalikwa. Timu nyingine ni Mauritius, Shelisheli,
Swaziland, Madagascar, Zimbabwe, Namibia,
Lesotho , Botswana, Malawi, Msumbiji, Zambia na wenyeji Afrika Kusini.
Kundi A lina timu za Namibia, Mauritius, Shelisheli na Zimbabwe, wakati Kundi B lina timu za Lesotho, Madagascar, Swaziland na Tanzania.
![]() |
| Tanzania imepangwa kundi mchekea B, pamoja na Lesotho, Madagascar na Swaziland Kundi A |
| Pos | Team | Pld | W | D | L | GF | GA | GD | Pts | |
|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
| 1 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | ||
| 2 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | ||
| 3 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | ||
| 4 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
Kundi B
| Pos | Team | Pld | W | D | L | GF | GA | GD | Pts | |
|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
| 1 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | ||
| 2 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | ||
| 3 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | ||
| 4 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
Mshindi wa kila kundi ataungana na wenyeji Afrika Kusini, Msumbiji, Zambia, Ghana, Botswana na Malawi kucheza Robo Fainali.
Kutakuwa na Nusu Fainali za aina mbili, kwanza za timu zilizofungwa katika Robo Fainali (Plate Semi Finas) na zilizoshinda (Semis Finals).
Vibonde wataendelea kupepetana hadi fainali yao ambayo itapigwa Mei 29, wakati fainali ya wakali itakuwa Mei 30.
![]() |
| Ghana ndiyo timu inayoongoza kwa ubora wa soka katika nchi zinazoshiriki COSAFA mwaka huu |
VIWANGO VYA UBORA;
Shelisheli ndiyo nchi duni zaidi kisoka kati ya timu zinazoshiriki COSAFA ya mwaka huu, ikiwa inashika nafasi ya 187, Mauritius 185, Swaziland 165, Madagascar 148, Zimbabwe 119, Namibia 111, Lesotho 125, Tanzania 107, Botswana 105,
Malawi 93, Msumbiji 90, Zambia 60, Afrika Kusini 56, wakati Ghana ndiyo ‘baba lao’ nafasi ya 25. Angola na Comoro zimejitoa.
RATIBA KAMILI COSAFA 2015
Mei 17, 2015
Namibia v Shelisheli (Saa 9:00 Alasiri, Uwanja wa Moruleng)
Zimbabwe v Mauritius (Saa 11:30 jioni Uwanja wa Moruleng)
Mei 18, 2015
Lesotho v Madagascar (Saa 11:30 jioni Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace)
Tanzania v Swaziland (Saa 1:30 usiku Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace)
Mei 19, 2015
Shelisheli v Zimbabwe (Saa 11:00 jioni Uwanja wa Moruleng)
Namibia v Mauritius (Saa 1:30 usiku Uwanja wa Moruleng)
Mei 20, 2015
Madagascar v Tanzania (Saa 11:00 jioni Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace)
Lesotho v Swaziland (Saa 1:30, usiku Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace)
Mei 21, 2015
Namibia v Zimbabwe (Saa 11:00 jioni Uwanja wa Moruleng)
Shelisheli v Mauritius (Saa 11:00 jioni Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace)
Mei 22, 2015
Lesotho v Tanzania (Saa 11:00 jioni Uwanja wa Moruleng)
Madagascar v Swaziland (Saa 11:00 jioni Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace)
![]() |
| Wenyeji Afrika Kusini wanapewa nafasi kubwa ya kubakiza taji nyumbani |
ROBO FAINALI
Mei 24, 2015
Ghana v Mshindi Kundi B (Saa 9:00 Alasiri Uwanja wa Moruleng)
Msumbiji v Malawi (Saa 11:30 Uwanja wa Moruleng)
Mei 25, 2015
Zambia v Mshindi Kundi A (Saa 11:30 Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace)
Afrika Kusini v Botswana (Saa 1:30 usiku Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace)
NUSU FAINALI ZA VIBONDE
Mei 27, 2015
Saa 11:00 jioni Uwanja wa Moruleng
Saa 1:30 usiku Uwanja wa Moruleng
FAINALI YA VIBONDE
Mei 29, 2015
Saa 11:00 jioni Uwanja wa Royal Bafokeng Sports Palace
NUSU FAINALI
Mei 28, 2015
Saa 11:00 jioni Uwanja wa Moruleng
Saa 1:30 usiku Uwanja wa Moruleng
MSHINDI WA TATU
Mei 30, 2015
Saa 9:00 Alasiri Uwanja wa Moruleng
FAINALI
Saa 11:30 jioni Uwanja wa Moruleng






.png)
0 comments:
Post a Comment