• HABARI MPYA

    Friday, May 22, 2015

    FIGO AJITOA KINYANG'ANYIRO CHA URAIS FIFA

    MWANASOKA wa zamani wa kimataifa wa Ureno, Luis Figo ametangaza kujitoa kwenye mbio za Urais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) unaotarajiwa kufanyika baadaye mwezi huu. 
    Rais wa Chama cha Soka Uholanzi, Van Praag naye mapema alijitoa na kutangaza kumuunga mkono Prince Ali bin Al Hussein, ambaye atapambana na Rais wa sasa, Sepp Blatter.
    Mwanasoka huyo wa zamani wa kimataifa wa Ureno amesema katika taarifa aliyotoa kwenye ukurasa wake Facebook kwamba; "Nimefanya uamuzi wangu, sitasimama katika huo unaoitwa uchaguzi huo wa FIFA. 
    Figo amesema kwamba alikubali kugombea Urais kwa FIFA inahitaji mabadiliko hayo haraka, lakini ameshuhudia mambo ambayo yanaweza kumtia aibu yeyote mmoja anataka anataka kuikomboa soka.
    Luis Figo announced his intention to stand for the FIFA presidency on Wednesday
    Luis Figo ametangaza kujitoa kuwania Urais wa FIFA 
    Figo won 127 international caps for his native Portugal and scored 32 goals
    Figo aliichezea timu yake ya taifa Ureno mechi 127 na kuifungia mabao 32 

    WASIFU WA LUIS FIGO

    Umri: Miaka 42 
    Klabu alizochezea:
    Sporting (1989–1995) - mechi 137, mabao 16
    Barcelona (1995–2000) - mechi 172, mabao 30
    Real Madrid (2000–2005) - mechi 164, mabao 38
    Inter (2005–2009)- mechi 105, mabao 9
    Mechi za kimataifa: 
    Mechi 127 Ureno, mabao 32
    Mataji na tuzo: 
    Barcelona - La Liga mawili, Copa del Reys mbili, Kombe la Washindi la UEFA moja, UEFA Super Cup moja,
    Real Madrid - La Liga mawili, Ligi ya Mabingwa moja, UEFA Super Cup moja
    Inter Milan - Serie A manne, Coppa Italia moja
    Tuzo binafsi: 
    Mwanasoka Bora wa Ureno kuanzia 1995 hadi 2000
    Ballon d'Or mwaka 2000
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: FIGO AJITOA KINYANG'ANYIRO CHA URAIS FIFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top