• HABARI MPYA

    Sunday, March 17, 2013

    ZOLA WA YANGA KUZIKWA KESHO KISUTU, MSIBA UPO JANGWANI

    Hamza Said 'Zola' enzi
    za uhai wake

    Na Mwandishi Wetu
    ALIYEKUWA mhudumu wa klabu ya Yanga SC, Hamza Said maarufu kama Zola au Chiluba aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo kwa ajali ya gari, anatarajiwa kuzikwa kesho Saa 10:00 jioni katika makaburi ya Kisutu, Dar es Salaam.
    Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh amesema kwamba kifo cha Hamza ni pigo kwa klabu, kwani alikuwa mchapakazi, mwaminifu na aliyejitolea mno kwa ajili ya klabu yake aipendayo.
    Alisema msiba upo makao makuu ya klabu, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani Dar es Salaam na ameomba wapenzi na wanachama kujitokeza kwa wingi kesho kumsindikiza mwenzao katika safari yake mwisho.
    Hamza alikutwa na umauti alfajiri ya leo, baada ya kugongwa na gari katika makutano ya Mitaa ya Rufiji na Kongo. Mungu aipumzishe roho ya marehemu mahala pema peponi. Amen
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: ZOLA WA YANGA KUZIKWA KESHO KISUTU, MSIBA UPO JANGWANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top