Wachezaji wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, wanaochezea klabu ya TP Mazembe ya DRC, Thomas Ulimwengu (kushoto) na Mbwana Samatta wakiwa uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasili jana tayari kwa kujiunga na kambi ya timu ya taifa kwa maandalizi ya kuikabili Morocco Jumapili hii katika mechi ya kuwania kucheza fainali za Kombe la Dunia mwakani. |