MANCHESTER United wamechapwa mabao 2-1 na Swansea City katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Liberty jioni ya leo.
Ander Herrera alianza kuwafungia wageni, United dakika ya 28 baada ya pasi ya Wayne Rooney, kufuatia kazi nzuri ya Angel di Maria.
Hata hivyo, shangwe za bao la United hazikudumu, baada ya Ki Sung-Yueng kuisawazishia Swansea dakika mbili baadaye akimalizia krosi ya Jonjo Shelvey, kabla ya Bafetimbi Gomis kuifungia la ushindi timu hiyo dakika ya 73.
Kikosi cha Swansea kilikuwa; Fabianski, Naughton, Fernandez, Williams, Taylor, Cork, Shelvey/Amat dk90, Ki 7, Sigurdsson/Montero dk74 na Gomis, Routledge.
Manchester United: De Gea, McNair/Valencia dk46, Jones, Rojo, Shaw/Young dk59, Blind, Herrera, Fellaini, Di Maria/Mata dk79, Rooney na Van Persie.
Kipa wa Manchester United, David de Gea akichupa bila mafanikio kujaribu kuzuia shuti la Sung-Yueng wa Swansea linalotinga nyavuni
PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2962915/Swansea-2-1-Manchester-United-Ki-Sung-Yueng-Bafetimbi-Gomis-seal-double-Louis-van-Gaal-s-form-side.html#ixzz3SOxysRRh
0 comments:
Post a Comment