• HABARI MPYA

    Wednesday, February 18, 2015

    ANELKA AMPELEKA CHELSEA POGBA, AMUAMBIA; "MAN UNITED USITHUBUTU"

    KIUNGO Paul Pogba ameshauriwa na Nicolas Anelka kuhamia Chelsea au Real Madrid ikiwa ataondoka Juventus mwishoni mwa msimu huu.
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 amesaini Mkataba mpya wa mshahara wa Pauni 70,000 kwa wiki na vigogo hao wa Serie A Oktoba mwaka jana ambao utamalizika Juni 2019.
    Lakini taarifa zinasema kwamba, kiungo huyo wa kimataifa wa Ufaransa, Pogba anataka kuondoka.
    French midfielder Pogba has been linked with some of the biggest clubs across Europe
    Kiungo wa Ufaransa, Paul Pogba anatakiwa na klabu kubwa mbalimbali Ulaya
    Nicolas Anelka (right) celebrates with Didier Drogba after scoring for Chelsea against Burnley in August 2009
    Nicolas Anelka (kulia) akishangilia na Didier Drogba baada ya kuifungia Chelsea dhidi ya Burnley Agosti mwaka 2009

    Na mshambuliaji wa zamani wa Chelsea na Real Madrid, Anelka, ambaye alicheza pamoja na Pogba katika mkopo wake wa miezi mitano Juventus mwaka 2013, anaamini kwamba Mfaransa huyo anapaswa kwenda Stamford Bridge au Santiago Bernabeu, kuliko kurejea Manchester United ambako alikaa kwa miaka mitatu.
    "Mtazamo wangu ni Chelsea, ambao hakika wana wachezaji wakubwa na nguvu ya kifedha ya [Roman] Abramovich au Real Madrid, ambao ni moja ya klabu kubwa duniani - ikiwa si kubwa kabisa.
    "Na ninaweza kuona yeye anafanya vizuri huko, pamoja na staili yake ya uchezaji na kocha wa huko, Carlo Ancelotti atapata mengi kutoka kwake. Kichwani mwake, Paul atakuwa tayari anafahamu klabu anayotaka kuchezea,"amesema Anelka.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ANELKA AMPELEKA CHELSEA POGBA, AMUAMBIA; "MAN UNITED USITHUBUTU" Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top