• HABARI MPYA

    Thursday, February 19, 2015

    LOGARUSIC ATUA KENYA KWA MADAHA; POSHO LIJE SASA

    Na Vincent Malouda, NAIROBI
    KOCHA wa zamani wa Simba SC ametua Kenya mchana wa leo kwa madaha ya aina yake akiwa amevalia miwani nzito ya jua.
    Mcroatia huyo ambaye aliteuliwa kocha mkuu wa klabu hiyo ya ligi kuu ya taifa la Kenya, AFC Leopards, ameshuka na ndege ya saa kumi na mbili unusu mchana kwenye uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta.
    Alipokelewa na mwenyekiti wa Leopards Allan Kasavuli na naibu katibu Profesa Asava Kadima waliyomvisha jezi ya klabu hiyo. Anatarajia kujiunga na timu ambayo kwa sasa ipo chini ya kocha msaidizi Yusuf Chippo kambini Mumias, magharibi mwa Kenya hivi leo jioni.
    Aliyekuwa kocha wa Simba SC, Zdravko Logarusic katika jezi ya AFC Leopards baada ya kuwasili Kenya
    Logarusic akiwa na viongozi wa AFC Leopard waliompokea Uwanja wa ndege wa Jomo Kenyata, Nairobi, Kenya leo

    Mechi yake ya kwanza itakuwa siku ya Jumamosi dhidi ya Chemelil Sugar katika uga wa Chemelil siku ambayo ligi kuu ya taifa itakuwa iking’oa nanga licha ya mgogoro unaoendelea na Shirikisho la Soka Kenya, FKF, kuhusu idadi ya timu zitakazoshiriki ligi kuu.
     ‘Loga’, ambaye tayari mashabiki wa AFC wamefurahia kurejea kwake Kenya, pia amezifunza klabu za Ashanti Gold na King Faisal FC za Ghana pamoja na wahasidi wa Leopards, Gor Mahia.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LOGARUSIC ATUA KENYA KWA MADAHA; POSHO LIJE SASA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top