IMEWEKWA JUNI 2, 2013 SAA 1:35 USIKU
KOCHA Sir Alex Ferguson alikuwa jukwaani akishuhudia magwiji wa Old Trafford wakimenyana na magwiji wa Real Madrid katika mchezo wa kirafiki wa hisani.
Bryan Robson aliiongoza timu hiyo ya England mbele ya mashabiki zaidi ya 60,000 ikilala 2-1 kwa Real Madrid.

Sir Alex Ferguson na Sir Bobby Charlton

Picha ya pamoja ya magwiji wa Real Madrid na Manchester United

Jaap Stam akipambana na Ruud van Nistelrooy, ambaye aliichezea kila timu kipindi kimoja

Zinedine Zidane akimtoka Denis Irwin
VIKOSI:
Manchester United: Van der Sar, van der Gouw; Berg, Blackmore, Irwin, Johnsen, Martin, Stam; Fortune, Robson, Scholes, Sharpe; Cole, van Nistelrooy, Yorke.
Real Madrid: Contreras, Sanchez; Cannavaro, Helguera, Hierro, Pavon, Salgado, Sanz; Amavisca, De la Red, Figo, McManaman, Makelele, Zidane; Alfonso, Butragueno, Morientes, van Nistelrooy.
Real Madrid: Contreras, Sanchez; Cannavaro, Helguera, Hierro, Pavon, Salgado, Sanz; Amavisca, De la Red, Figo, McManaman, Makelele, Zidane; Alfonso, Butragueno, Morientes, van Nistelrooy.
Mshambuliaji wa zamani wa Liverpool, Fernando Morientes aliifungia bao la kwanza Real na Ruud van Nistelrooy, ambaye aliichezea kila timu kipindi kimoja, akaisawazishia United.
Sekunde kadhaa baada ya Dwight Yorke kugongesha mpira kwenye mwamba wa juu, Ruben de la Red akafunga bao la ushindi zikiwa zimesalia dakika tano.
Edwin van der Sar alikuwa bora alikuwa nyota wa mchezo kwa upande wa United kwa kuokoa michomo kadhaa ya hatari kabla ya kumpisha Raymond van der Gouw kipindi cha pili.

Ruud van Nistelrooy baada ya kuifungia United

Magwiji wa Real Madrid wakimpongeza Fernando Morientes

Dwight Yorke akipiga shuti pembeni ya Francisco Pavon

Claude Makelele akipambana na Paul Scholes

Edwin van der Sar aliokoa sana

Andy Cole alidhibitiwa

Fernando Hierro na Denis Irwin walikuwa Manahodha


.png)