TIMU ya Bayern Munich jana ililazimishwa sare ya kufungana mabao 3-3 na RB Leipzig katika mchezo wa Bundesliga Uwanja wa Allianz Arena Jijini Munich.
Mabao ya Bayern Munich yalifungwa na Jamal Musiala dakika ya 30 na Thomas Muller mawili, dakika ya 34 na 75, wakati ya RB Leipzig yalifungwa na Christopher Nkunku dakika ya 19, Justin Kluivert dakika ya 36 na Emil Forsberg dakika ya 48.
Kwa matokeo hayo, Bayern Munich inaendelea kuongoza Bundesliga kwa pointi mbili zaidi ya RB Leipzig (23-21) baada ya wote kucheza mechi 10 PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment