• HABARI MPYA

    Thursday, December 24, 2020

    MAN UNITED KUMENYANA NA MAN CITY NUSU FAINALI CARABAO CUP

    MANCHESTER United ilitumia dakika mbili za mwsho kujikatia tiketi ya Nusu Fainali ya Kombe la Ligi England, maarufu kama Carabao Cup kwa mabao ya Edinson Cavani dakika ya 88 na Anthony Martial dakika ya 90 na ushei ikiwalaza wenyeji, Everton 2-0 Uwanja wa Goodison Park. 
    Mechi nyingine ya Robo Fainali ya Carabao Cup jana, Tottenham Hotspur iliwachapa wenyeji wengine, Stoke City 3-1 Uwanja wa bet365, Stoke-on-Trent, Staffordshire.
    Ikumbukwe jana Manchester City iliichapa Arsenal 4-1 Uwanja wa Emirates, London na Brentford ikichapa Newcastle United 1-0 Uwanja wa Brentford Community.
    Sasa Manchester United itacheza na Manchester City katika Nusu Fainali Januari 5, 2021 uwanja wa Old Trafford, wakati Tottenham Hotspur itamenyana na Brentford 


    NUSU FAINALI: Januari 5, 2021
    Saa 8:00 mchana
    Manchester United Manchester City
    Saa 2:00 usiku
    Tottenham Hotspur Brentford

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED KUMENYANA NA MAN CITY NUSU FAINALI CARABAO CUP Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top