• HABARI MPYA

    Wednesday, January 29, 2014

    KIPRE TCHETCHE AMKAMATA TAMBWE KWA MABAO LIGI KUU, AZAM INOGILEEE CHAMAZI

    MFUNGAJI bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu uliopita, Kipre Herman Tchetche amefunga bao lake la 10 msimu huu hivyo kulingana na mchezaji aliyekuwa anaongoza kwa muda mrefu, Amisi Tambwe wa Simba SC. 
    Raia huyo wa Ivory Coast, amefunga bao la kipindi cha kwanza timu yake ikiwa inaongoza  1-0 hadi sasa Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam hadi sasa.
    Kipre sasa akiwa anafungana na Mrundi Tambwe, wanafuatiwa kwa karibu na Elias Maguri wa Ruvu Shooting na Juma Luizio wa Mtibwa Sugar wenye mabao nane kila mmoja.  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KIPRE TCHETCHE AMKAMATA TAMBWE KWA MABAO LIGI KUU, AZAM INOGILEEE CHAMAZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top