Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
AMISI Tambwe leo ameinua mikono miwili juu akiikunja mithili ya ngumi- baada ya kufunga bao la 10 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Ashanti United na kuendelea kuongoza kwa mabao katika ligi hiyo.
Alikuwa anamaanisha 10- yaani mabao 10 katika mechi 11 alizocheza msmu huu na sasa Mrundi huyo anamzidi kwa mabao mawili, Mganda Hamisi Kiiza wa Yanga mwenye mabao manane sawa na Juma Luizio wa Mtibwa Sugar na Elias Maguri wa Ruvu Shooting.
Mfungaji bora wa Ligi Kuu msimu uliopita, Kipre Herman Tchetche wa Azam FC, raia wa Ivory Coast ana mabao saba sawa na Themi Felix wa Kagera Sugar, wakati Mrisho Ngassa ana mabao matano sawa na Didier Kavumbangu anayecheza naye Yanga SC na Tumba Swedi wa Ashanti United, ambaye ndiye beki mwenye mabao mengi zaidi msimu huu hadi sasa.
Kiiza na Kipre Tchetche wana nafasi za kuongeza mabao watakapokuwa wakizichezea timu zao kesho mechi za mwisho za mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu, Yanga ikimenyana na JKT Oljoro na Azam FC na Mbeya City.
WAFUNGAJI WA MABAO LIGI KUU:
JINA TIMU MABAO
Amisi Tambwe Simba SC 10
Hamisi Kiiza Yanga SC 8
Juma Luizio Mtibwa 8
Elias Maguri Ruvu Shoot 8
Kipre Tchetche Azam FC 7
Themi Felix Kagera 7
Mrisho Ngassa Yanga SC 5
Tumba Swedi Ashanti 5
D. Kavumbangu Yanga SC 5
AMISI Tambwe leo ameinua mikono miwili juu akiikunja mithili ya ngumi- baada ya kufunga bao la 10 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Ashanti United na kuendelea kuongoza kwa mabao katika ligi hiyo.
Alikuwa anamaanisha 10- yaani mabao 10 katika mechi 11 alizocheza msmu huu na sasa Mrundi huyo anamzidi kwa mabao mawili, Mganda Hamisi Kiiza wa Yanga mwenye mabao manane sawa na Juma Luizio wa Mtibwa Sugar na Elias Maguri wa Ruvu Shooting.
![]() |
| Salamu kwa Kiiza; Amisi Tambwe akionyesha ngumi mbili kumaanisha mabao 10 aliyofikisha leo |
Mfungaji bora wa Ligi Kuu msimu uliopita, Kipre Herman Tchetche wa Azam FC, raia wa Ivory Coast ana mabao saba sawa na Themi Felix wa Kagera Sugar, wakati Mrisho Ngassa ana mabao matano sawa na Didier Kavumbangu anayecheza naye Yanga SC na Tumba Swedi wa Ashanti United, ambaye ndiye beki mwenye mabao mengi zaidi msimu huu hadi sasa.
Kiiza na Kipre Tchetche wana nafasi za kuongeza mabao watakapokuwa wakizichezea timu zao kesho mechi za mwisho za mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu, Yanga ikimenyana na JKT Oljoro na Azam FC na Mbeya City.
WAFUNGAJI WA MABAO LIGI KUU:
JINA TIMU MABAO
Amisi Tambwe Simba SC 10
Hamisi Kiiza Yanga SC 8
Juma Luizio Mtibwa 8
Elias Maguri Ruvu Shoot 8
Kipre Tchetche Azam FC 7
Themi Felix Kagera 7
Mrisho Ngassa Yanga SC 5
Tumba Swedi Ashanti 5
D. Kavumbangu Yanga SC 5



.png)
0 comments:
Post a Comment