• HABARI MPYA

    Thursday, October 24, 2013

    YAYA TOURE AKUMBANA NA UBAGUZI URUSI, AIWAKIA UEFA KUSHINDWA KUWALINDA WEUSI ULAYA

    KIUNGO Yaya Toure amekumbana na kejeli za kibaguzi akifananishwa na nyani usiku huu Manchester City ikiibuka na ushindi wa 2-1 ugenini dhidi ya CSKA Moscow katika Jiji Kuu la Urusi.
    Kelele za kibaguzi zilisikika kutoka mashabiki wa wenyeji katika mchezo ambao City ilinufaika na mabao mawili ya Sergio Aguero ikitoka nyuma na kushinda mechi hiyo ya Li ya Mabingwa Ulaya.
    Na City imethibitisha itapeleka malalamiko rasmi UEFA juu ya 'unyama' aliofanyiwa Toure. 
    "Hakika inaumiza mtu unapozungumza na watu wanaendelea kufanya hivyo,"alilalamika Toure. "Huwezi kuamini na inaniumiza sana upande wangu,".
    Unawasikia wale? Yaya Toure akimuambia refa Ovidiu Hategan juu ya mashabiki waliokuwa wakimuita nyani
    Upset: Toure gestures towards the fans
    Inauma: Toure akiwastaajabu mashabiki wabaguzi
    Time to act: Toure has called on UEFA to take action against fans who racially abuse players
    Toure ameitaka UEFA kuchukua hatua kali
    Target: Yaya Toure received racist abuse from sections of the crowd in Moscow
    Mlengwa: Yaya Toure alikumbana na kejeli za kibaguzi kutoka mashabiki mjini Moscow

    Respect: Toure wore a 'No to racism' armband
    Heshima: Toure alivaa beji ya kupiga ubaguzi
    "Nafikiri UEFA wanahitaji kufanya kitu cha nguvu. Itakuwa vizuri ikiwa watazuia hiyo.
    "Baadhi ya nyimbo zilizokuwa zinaimbwa zilikuwa za kipumabvu kabisa, nafikiri UEFA wanatakiwa kufanya kazi. Kila wakati tunasema kitu fulani na inaendelea, kitu fulani lazima kifanyika kuzuia hii,".
    Alipoulizwa ni hatua gani ichukuliwe na bodi hiyo ya soka Ulaya, Toure alitaka adhabu zitolewe badala ya faini ndogo ndogo ambazo zimekuwa zikitolewa siku za nyuma.
    "Wanahitaji kufanya zaidi,"alisema. "Nafikiri UEFA wanatakiwa kuwa na nguvu, na kuzishika klabu zote na mashabiki wote wanaofanya hivyo (wahusika). Labda kufungia viwanja,".
    "Kwangu kama mchezaji wa Afrikan wakati wote imezungumzwa kusikia kwamba mambo kama hayo tunahitaji kufanya kitu juu ya hilo,".
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YAYA TOURE AKUMBANA NA UBAGUZI URUSI, AIWAKIA UEFA KUSHINDWA KUWALINDA WEUSI ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top