![]() |
| Meneja wa Kilimanjaro, George Kavishe akimkabidhi jezi Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Simba SC, Joseph Itangare 'Kinesi' kulia |
Na Ibrahim Kyaruzi, IMEWEKWA JUNI 5, 2013 SAA 9:30 ALASIRI
IKIWA ni sehemu ya udhamini wake, bia ya Kilimanjaro Premium Lager imewapa
vifaa vya michezo Simba na Yanga kwa ajili ya michuano wa Kombe la Kagame
iliyopangwa kufanyika kuanzia tarehe 18 Juni mwezi huu.
Akikabidhi vifaa hivyo Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George
Kavishe alisema, ‘‘ Bila ubishi Simba na Yanga ndio klabu kubwa za mpira
Tanzania na zote zimefika katika fainali
za mchuano wa Kombe la Kagame kwa mara ya
19 sasa, haya ni mafanikio makubwa kwa hizi timu, kama wadhamini wakuu
wa timu hizi, Kilimanjaro Premium Lager
inaziunga mkono Simba na Yanga katika harakati zao kucheza tena fainali
za michuano hii ya kusisimua na ya kihistoria.
![]() |
| Kavishe akimkabidhi jezi Katibu wa Yanga SC, Lawrence Mwalusako |
Aliongeza kuwa Kombe la Kagame ni
mashindano makubwa Africa mashariki na kati, na ni jukwaa bora kwa wachezaji
wetu kuonyesha vipaji vyao dhidi ya
wachezaji wa viwango vya juu katika kanda hii lakini pia ni jukwaa zuri kwa
wale wanaounda timu za taifa kuchagua wachezaji.
“Ushirikiano huu baina ya Bia ya Kilimanjaro na klabu hizi ni mizizi
inayotokana na maadili katika kazi, kufanya kazi kama timu na ile kiu ya
mafanikio. Na mafanikio ya ushirikiano
huu ni pamoja na kushuhudia mara kwa
mara timu hizi mbili zikitoa
wachezaji kwa timu ya Taifa (Taifa Stars) ambao wamekuwa na matokeo mazuri chini ya udhamini
wa Bia ya Kilimanjaro.
Tutaendelea kusaidia timu hizi, na kuhakikisha tunapeleka mpira wa
nchi hii kwenye kilele cha mafanikio.
Meneja wa Bia ya Kilimanjaro pia aliwataka
Simba na Yanga kuhakikisha wanaiwakilisha nchi yetu vizuri katika mchuano huu mkubwa wa vilabu katika
ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na kuwasihi kuchukua ushindi na kurudi na kombe la 12 la Kagame
kwa mashabiki wanaosubiria kwa hamu.




.png)