• HABARI MPYA

    Friday, April 19, 2013

    MAMA AMUWEKA SOKONI CAVANI, CHELSEA NA MAN CITY WASHINDWE WENYEWEEEEE


    MSHAMBULIAJI hatari wa Napoli, Edinson Cavani, imeelezwa anauzwa na mama yake wakati wa mahojiano na kituo cha Radio cha Uruguay.
    Manchester City na Chelsea zimekuwa zikimtolea macho mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, ambaye ana thamani ya Pauni Milioni 53.
    Katika mahojiano hayo, mama yake Berta Gomez, amesema: "Ameniambia anataka kwenda sehemu nyingine na kuondoka Napoli.
    Pricey: Edinson Cavani has become one of Europe's most deadly strikers
    Kifaa: Edinson Cavani amekuwa mmoja wa washambuliaji gumzo duniani

    "Edi bado hajui nini kitatokea, Napoli ni mji wa soka. Watu wamechanganyikiwa na soka ajabu na wakati wote nimekuwa nikimuambia mwanangu: unaweza kwenda popote, lakini hakuna atakayekupenda kama wanavyofanya Napoli.'
    Cavani amesema itakuwa vigumu kubaki katika klabu hiyo kama watashindwa kumshawishi kwa kuboresha kikosi ili kiweze kushinda mataji makubwa.
    Kama ilivyo kwa klabu nyingi za England, Real Madrid inasadikiwa kuwa kinara wa mbio za kuwania saini ya mshambuliaji huyo.
    World class: He is good enough to be a success in England or Spain
    Kiwango cha dunia: Ni mzuri kiasi cha kutosha kupata mafanikio England au Hispania
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments
    Item Reviewed: MAMA AMUWEKA SOKONI CAVANI, CHELSEA NA MAN CITY WASHINDWE WENYEWEEEEE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top