BAO pekee la kujifunga la Craig Dawson dakika ya 53 jana liliipa Manchester United ushindi wa 1-0 dhidi ya West Ham United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Old Trafford.
Kwa ushindi huo, Mmanchester United inafikisha pointi 57 baada ya kucheza mechi 29, ingawa inabaki nafasi ya pili, sasa ikizidiwa pointi 14 na jirani zao, Manchester City ambao hata hivyo wamecheza mechi moja zaidi PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment