TIMU ya Real Madrid jana iliibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Elche katika mchezo wa Ligi Kuu ya Hispania Uwanja wa Alfredo Di Stefano Jijini Madrid.
Mabao ya Real Madrid yalifungwa na Karim Benzema yote dakika ya 73 na 90 na ushei, wakati la Elche lilifungwa na Dani Calvo dakika ya 61 na kwa ushindi huo timu ya kocha Zinadine Zidane inafikisha pointi 57 baada ya kucheza mechi 27 na kurejea nafasi ya pili, ikiizidi pointi moja Barcelona ambayo imecheza mechi 26 PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment