• HABARI MPYA

    Tuesday, December 30, 2014

    PSPF KUWAKUTANISHA WACHEZAJI WA ZAMANI WA YANGA NA SIMBA

    Na Abdul Njaidi, DAR ES SALAAM
    MFUKO wa Pensheni wa PSPF umedhamini mchezo wa kirafki utakaowakutanisha wachezaji waliowahi kuwika katika timu kongwe nchini Simba na Yanga.
    Mchezo huo unatarajiwa kufanyika tarehe 1 Januari 2015 katika  uwanja wa chuo cha Bandari, Tandika jijini Dar es Salaam,  kiingilio kitakuwa bure ikiwa ni zawadi ya mwaka mpya kutoka PSPF.   
    Katika mchezo huo baadhi ya wachezaji wa Simba wanaotarajiwa kushuka uwanjani ni Thomas Kipese, George Lucas, Bita John, George Masatu, Mustafa Hoza, Emmanuel Gabriel, Idd seleman. Timu ya Simba inafanya mazoezi katika uwanja wa Leaders uliopo Kinondoni, ipo chini kocha mchezaji Kasongo Athuman. 
    Abubakar Salum 'Sure Boy' akimtoka Iddi Selemani wa Simba SC enzi zao wakicheza. Wakali hao watakumbushia enzi wiki hii 

    Wanaotarajiwa kushuka uwanjani kwa upande wa  Yanga ni Peter Manyika, Mwanamtwa Kihwelo, Edibily Lunyamila, Mohamed Husein, Chibe Chibindu, Aboukar Salum, Bakari malima. Yanga wanafanya mazoezi katika uwanja wa kauda ulipo katika makao makuu ya klabu hiyo kariakoo Jijini Dar es Salaam, wakiongozwa na kocha Peter Tino.
    Lengo la mchezo huo ni kutoa burudani kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na maeneo ya karibu hususani katika kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka. PSPF itatumia fursa hiyo kutangaza huduma zake mpya ambazo Mkopo wa Elimu na Mkopo wa Kuanza Maisha. Tunatoa mwito kwa wapenzi wa soka kujitokeza kwa wingi katika mchezo huo ili kuwaona wakongwe waliowahi kutikisha nchi katika anga ya soko nchini.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PSPF KUWAKUTANISHA WACHEZAJI WA ZAMANI WA YANGA NA SIMBA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top