Chedjou hajaichezea nchi yake tangu Kombe la Dunia mwaka huu, lakini kuumia goti kwa Nlate katika ajali ya gari kiasi cha kutoweza kushiriki michuano hiyo ya timu 16 Equatorial Guinea kuanzia Januari 17 kunamrudisha kikosini.
Chedjou mwenye umri wa miaka 29, anayechezea Galatasaray ya Uturuki, ni miongoni mwa wachezaji wakongwe ambao muda wao kuichezea timu ya taifa ulionekana kupita, baada ya Cameroon kufungwa mechi zote tatu za kundi lake kwenye Kombe la Dunia Brazil.
0 comments:
Post a Comment