• HABARI MPYA

    Monday, November 11, 2013

    MESSI AUMIA TENA, LAKINI BARCA YASHINDA 4-1 BILA YEYE...AMEUMIA KIAJABU!

    KLABU ya Barcelona ilimudu kushinda 4-1 dhidi ya Real Betis licha ya Lionel Messi kuumia mapema.
    Messi alipata matatizo wakati akikimbia na mpira dakika ya 18 - majeruhi ya tatu ya mguu wake msimu huu.
    Neymar na Pedro walifunga mabao mawili ndani ya dakika mbili kipindi cha kwanza na Cesc Fabregas akakamilisha ushindi mnono kwa mabao mawili ya kipindi cha pili, kabla ya Jorge Molina kuifungia kwa penalti Betis dakika za majeruhi.
    Barcelona imesema kwamba Messi ana matatizo ya misuli na atakwenda kufanyiwa vipimo leo. Mwanasoka huyo bora mara nne wa dunia nafasi yake ilichukuliwa na Andres Iniesta dakika ya 21.

    Wasiwasi wa majeruhi: Lionel Messi aliumia wakati anakimbia na mpira kabla ya kutolewaNo problem: But Barca were able to overcome his injury and went on to win 3-0
    Hakuna tatizo: Lakini Barca ilishindaOn target: Neymar, Pedro and two from Cesc Fabregas sealed the victory
    Wamefunga: Mabao ya Neymar, Pedro na mawili ya Cesc Fabregas waliipa timu hiyo ushindi mnonoInjury: Messi picked up his injury while sprinting for the ball
    Withdrawal: But he was substituted after just 21 minutes
    Anatoka: Alitolewa dakika ya 21
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MESSI AUMIA TENA, LAKINI BARCA YASHINDA 4-1 BILA YEYE...AMEUMIA KIAJABU! Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top