• HABARI MPYA

    Saturday, April 26, 2014

    VAN GAAL AMTEUA KLUIVERT KOCHA MSAIDIZI WAKE MAN UNITED

    KOCHA Luis van Gaal anajiandaa kumchukua Patrick Kluivert akawe msaidizi wake atakapojiunga na Manchester United.
    Kwa mujibu wa gazeti la De Telegraaf na Uholanzi, ambalo lina ukaribu na kambi ya Van Gaal, kocha huyo tayari amejihakikishia kazi Old Trafford. 
    BIN ZUBEIRY inafahamu ulifanyika mkutano siku chache zilizopita baina ya wawakilishi wa Van Gaal na United.
    Makocha wapya Old Trafford? Louis van Gaal atamchukua Patrick Kluivert akawe Msaidizi wake Man United
    Legend: Kluivert played under Van Gaal for Ajax and Barcelona (above)
    Gwiji: Kluivert alikuwa mchezaji wa Van Gaal katika klabu za Ajax na Barcelona 

    United imekanusha madai ya kufikia makubaliano, lakini gazeti pia limesema Kluivert - kwa sasa anafanya kazi chini ya Van Gaal katika timu ya taifa ya Uholanzi- anaweza kurithi mikoba iwapo Van Gaal ataondoka.
    Mshambuliaji huyo wa zamani wa kimataifa wa Uholanzi alicheza chini ya Van Gaal katika klabu za Ajax na Barcelona kabla ya kusajiliwa na Newcastle mwaka 2004.
    Kocha wa makipa, Frans Hoek na mchua misuli, Jos van Dijk pia wanatajwa kuwamo katika timu ya Van Gaal ya benchi la Ufundi atakayohamia nayo United.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: VAN GAAL AMTEUA KLUIVERT KOCHA MSAIDIZI WAKE MAN UNITED Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top