• HABARI MPYA

    Wednesday, April 23, 2014

    CHELSEA YAKOMAA NA WABABE WA BARCA UGENINI, NGOMA DROO

    CHELSEA imelazimisha sare ya bila kufungana na Atletico Madrid katika Nusu Fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku huu Uwanja wa Vicente Calderon 
    Maana yake, Chelsea itahitaji ushindi mwembamba katika mchezo wa marudiano Uwanja wa Stamford Bridge, London dhidi ya timu iliyoitoa Barcelona katika Robo Fainali ili kutinga Fainali. 
    Chelsea leo ilimpoteza kipa wake wa kwanza Petr Cech mapema dakika ya 17 baada ya kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na Schwarzer aliyemalizia vizuri mchezo.
    11 wa ukweli: Kikosi cha Chelsea kilichotoa sare ya 0-0 ugenini na timu ngumu ya Atletico Madrid usiku huu  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: CHELSEA YAKOMAA NA WABABE WA BARCA UGENINI, NGOMA DROO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top