MABAO ya Marcus Rashford dakika ya 31 na Bruno Fernandes dakika ya 90 usiku huu yameipa Manchester United ushindi wa 2-0 dhidi ya wenyeji, Granada katika mchezo wa kwanza wa Robo Fainali UEFA Europa League Uwanja wa Nuevo Los Cármenes Jijini Granada.
Timu hizo zitarudiana Aprili 15 Uwanja wa Old Trafford na mshindi wa jumla atakutana na mshindi wa jumla kati ya Ajax na AS Roma. Leo Roma imewafunga Ajax 2-1 Jijini Amsterdam.
0 comments:
Post a Comment