KIUNGO mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Idd Suleiman 'Nado' amesaini mkataba mpya wa miaka miwili kuendelea kuichezea Azam FC.
Nado alisaini mkataba huo jana mchana mbele ya Ofisa Mtendaji Mkuu, Abdulkarim Amin 'Popat', utakaomfanya aendelee kusalia Azam FC hadi mwaka 2024.
Nado aliyejiunga na Azam FC msimu uliopita akitokea Mbeya City, amekuwa mchezaji muhimu kikosini na hadi sasa msimu huu akiwa amehusika kwenye mabao 12 ya timuhiyo, akifunga mara saba na kutoa pasi za mwisho tano.
0 comments:
Post a Comment