• HABARI MPYA

    Wednesday, April 01, 2020

    LIGI YA MABINGWA NA EUROPA LEAGUE ZASOGEZWA HADI AGOSTI

    HATUA zijazo za michuano ya  Ligi ya Mabingwa Ulaya na Europa League zimeripotiwa kusogezwa hadi Julai na Agosti kutokana na janga la maambukizi ya virusi vya corona linaloendelea duniani kote. 
    Mechi zote za timu za taifa zilizopangwa kuchezwa Juni zimeahirishwa ili kuupisha msimu wa 2019-20 ukamilishwe.
    Taarifa hiyo imetolewa na Shirikisho la Soka Ulaya (UEFA) baada ya mkutano uliofanyka kwa video leo. 
    Mechi, mashindano na ligi zote za soka Ulaya zimesitishwa tangu katikati ya Machi kutokana na mlipuko wa virusi vya corona, ulioanzia Wuhan huko China mwishoni mwa mwaka jana.

    Michuano ya  Ligi ya Mabingwa Ulaya na Europa League imesogezwa mbele hadi Julai na Agosti kutokana na janga la maambukizi ya virusi vya corona 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LIGI YA MABINGWA NA EUROPA LEAGUE ZASOGEZWA HADI AGOSTI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top